Jeshi la Polisi Tanzania limeimarisha ulinzi na kuongeza doria katika maeneo mbalimbali ikiwamo vituo vya mwendokasi, maeneo ya makutano ya barabara, maeneo yenye misongamano ya watu kama kariakoo katika kile kinachotazamwa ni hatua ya kuzua maandamano yaliyopangwa kufanyika Julai 7. Magari ya polisi pia yameonekana yakizunguka sehemu mbalimbali jijini Dar es salaam na ripoti zinasema maafisa wa serikali wakiwa na askari wamekuwa wakifanya ukaguzi wa kushtukiza katika sehemu za kulala wageni.
Jeshi la Polisi Tanzania laimarisha ulinzi Dar es Salaam