Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Dereva wa Gari ya Serikali Akamatwa Akiendesha Huku Amelewa

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, wamemkamata dereva wa gari la Serikali aliyekuwa akiendesha akiwa amelewa, kitendo kinachodaiwa kuhatarisha usalama wa abiria na watumiaji wengine wa barabara.

Dereva huyo alikamatwa wakati wa ukaguzi wa mabasi uliofanyika jana mkoani Kilimanjaro, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha usalama barabarani na kudhibiti ajali.

Akizungumza baada ya kukamatwa kwa dereva huyo, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Kilimanjaro, ACP Nassoro Sisiwayah, amesema Jeshi la Polisi halitavumilia madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani, hususan wanaoendesha vyombo vya moto wakiwa wamelewa.

Ameongeza kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya madereva wote wenye tabia kama hiyo, akisisitiza kuwa vyombo vya dola vimejipanga kudhibiti vitendo vinavyoweza kusababisha ajali na kuhatarisha maisha ya wananchi.

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: