Mwanasheria mkuu wa Tanzania Hamza Johari amekula kiapo cha kazi Jumatano ya tarehe 05/11/2025 katika ikulu ya Chamwino Dodoma.
Hamza Said Johari aliteuliwa siku ya Jumatatu na Rais Samia Suluhu baada ya kuingia ikulu kwa muhula wa pili utakaokamilika 2030.
Viongozi mbalimbali wamehudhuria hafla hiyo ya uapisho wa mwanasheria mkuu wakiongozwa na Rais Samia Suluhu.
Aliyeongoza uapisho huo ni Jaji mkuu George Mcheche Masaju.
Mwanasheria mkuu huyu pia alikuwa katika wadhifa huo muhula uliopita wa Rais Samia.
Kabla ya kuwa Mwanasheria mkuu wa serikali ya muungano wa Jamhuri ya Tanzania alikuwa mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya usafiri wa anga Tanzania.
Kwa mujibu wa Ibara ya 112(1)(b), Mwanasheria Mkuu wa Serikali atakuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kati ya Wajumbe Sita.
Chanzo; Bbc