Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Amuua Mpenzi Wake Kisha na Yeye Kujinyonga Kisa Wivu wa Mapenzi

Wivu wa kimapenzi umesababisha vifo vya watu wawili mkoani Mwanza, baada ya tukio la mauaji lililotokea wilaya ya Magu. Desemba 27 mwaka huu ambapo Marietha Kalafala (33), mfanyakazi wa Kiwanda cha Ziwa Steel na mkazi wa Kitongoji cha Mwabuyi, aliuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali katika shingo, mgongo na paji la uso na mwili wake kisha kutupwa kwenye shamba la mahindi.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa mauaji hayo yalifanywa na mpenzi wake, Wilbert Yona (34), mfanyakazi wa Kiwanda cha Ziwa Steel. Baada ya tukio hilo, Desemba 28 majira ya saa 3 asubuhi, Wilbert alijinyonga ndani ya nyumba ya kulala wageni iliyopo Kata ya Nyanguge, Wilaya ya Magu, ikidaiwa ni ili kuepuka hatua za kisheria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbrod Mtafungwa, amesema miili ya marehemu wote wawili imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Lugeye kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu na kisha itakabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi.

 

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: