Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Askofu Ruwa’ichi Hali ya Askofu Pengo Sio Nzuri

Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Juda Thaddeus Ruwa’ichi, amesema hali ya afya ya Kardinali Policarp Pengo, sio nzuri kutokana na changamoto za kiafya zinazomkabili.

Taarifa ya Askofu Ruwa’ichi iliyotolewa leo, imetoa wito kwa Wakatoliki kumwombea Kardinali Pengo.

“ Mzee wetu mpendwa Kardinali Policarp Pengo anakabiliwa na changamoto za kiafya. Zimefanyika jitihada za kumsaidia kimatibabu hapa kwetu. Hata hivyo, imeonekana kwamba upo uhitaji wa kumpeleka nje ili apate matibabu ya uhakika zaidi.

“Kwa hiyo, mipango imefanyika ili akatibiwe India. Tunatarajia kwamba ataondoka siku za usoni kwa lengo la matibabu hayo. Ninawaalika nyote tuungane kumsindikiza kwa sala na matashi mema,” amesema Askofu Ruwa'ichi

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: