Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Aboubakar Afariki Azama Ziwani, Mwili wa Mwanaume Miaka 40 Wapatikana

kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna Wilbrod Mutafungwa amesema tarehe 24 mwezi wa pili mwaka huu katika mtaa wa Bushata kisiwa cha Bezi majira ya saa mbili usiku mvuvi aitwaye Aboubakar Shaban Ramadhan (44) alizama ziwani na kupoteza maisha wakati akiendelea na shughuli zake za uvuvi

Tukio la pili limetokea Machi 1, 2026 majira ya saa 2:00 asubuhi katika Mtaa wa Mtakuja, Kata ya Nyamhongolo, Wilaya ya Ilemela, ambapo ulipatikana mwili wa mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 40 hadi 50.

Kamanda Mutafungwa amesema mwili huo ulikutwa katika shamba la miwa lililopo kwenye bonde la Mto Maji ya Rangi na uchunguzi wa awali unaonesha huenda marehemu alisombwa na maji kutoka eneo jingine kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kushindwa kuhimili nguvu ya maji.

 

 

Chanzo; Clouds Media

Kuhusiana na mada hii: