Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Nurdin Bilal Juma maarufu ‘Shetta’, leo Jumatano, Machi 4, 2026, amezindua mpango maalum unaolenga kusafisha jiji, ambao unatarajiwa kuchangia uzalishaji wa ajira mpya 300,000.
Mpango huo unalenga kubadili taka zinazozalishwa na kuzirudisha katika mnyororo wa uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, ikiwemo gesi ya kaboni.
Kuelekea utekelezaji wa mpango huo, Mstahiki Meya amesema malengo ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ni kutengeneza ajira 300,000 ndani ya kipindi cha miaka mitano, yaani hadi kufikia mwaka 2030.
Chanzo; Global Publishers