Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Heche Ajimwa Dhamana

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Makamu Mwenyekiti Taifa, John Heche anashikiliwa kwenye mahabusu ya jeshi la Polisi Mtumba jijini Dodoma lakini amenyimwa dhamana.

Katika taarifa iliyotolewa na chama hicho kwa vyombo vya habari jana, ilieleza kuwa licha ya mawakili wa chama hicho kufika kumpa msaada wa kisheria lakini walinyimwa kumuwekea dhamana.

Heche alikamatwa na Jeshi la Polisi siku ya Jumatano kwenye lango la kuingilia Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam kabla ya kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es salaam kisha kusema wanampeleka mkoani Mara hata hivyo mawakili na ndugu wa kiongozi huyo walipomfuatilia katika vituo vya polisi mkoani Mara hawakufanikiwa kumuona.

 

Chanzo: Nipashe

Kuhusiana na mada hii: