Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Zanzibar Kuanza Kupiga Kura

Ni dhahiri safari ya siku 46 za kampeni za kuusaka urais, ubunge, uwakilishi na udiwani kisiwani Zanzibar imekamilika baada ya kuhitimishwa leo Jumatatu, Oktoba 27, 2025.

Kukamilika kwa kampeni hizo kunatoa nafasi kwa wananchi kupiga kura ya mapema kesho Jumanne, Oktoba 28, 2025, kabla ya kura kuu itakayojumuisha wapigakura wote keshokutwa, Oktoba 29.

Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), wapigakura 717,557 wanatarajiwa kupiga kura, kati ya hao wanawake ni 378,334 sawa na asilimia 53, na wanaume ni 339,223 sawa na asilimia 47

“Kati ya idadi hiyo, wenye umri kati ya miaka 18 hadi 35 ni 326,304 sawa na asilimia 45, wenye umri wa miaka 36 hadi 59 ni 300,986 sawa na asilimia 42, na wenye umri kuanzia miaka 59 na kuendelea ni 90,267 sawa na asilimia 13,” amesema Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar, Thabit Idarous Faina.

Kwa mujibu wa Sheria Namba Nne ya Uchaguzi ya mwaka 2018, imeelezwa kuwa kura ya mapema hufanyika kabla ya uchaguzi mkuu. Kura hiyo inawahusu watendaji wote wanaoshughulika na uchaguzi, walinzi na wasimamizi wa siku ya uchaguzi, ili waweze kutimiza majukumu yao bila changamoto zozote.

Safari ya kufikia hatua hiyo ya kupiga kura ilianza kwa mchakato wa kuwapata wagombea, kuteuliwa na kupitishwa na ZEC kuwania nafasi hizo.

Kwa mujibu wa Faina, tume imehidhinisha eneo moja la kupigia kura ya mapema kwa kila jimbo, hivyo kutakuwa na maeneo 50, Unguja ikiwa na vituo 32 na Pemba 18. Hata hivyo, katika maeneo hayo kutakuwa na vituo 407 kwa shehia zote 388, zikiwamo shehia za ziada.

Pia, imeidhinisha vituo vya kupigia kura 1,752; kati ya hivyo, Unguja ni 1,294 na Pemba ni 458, kwa ajili ya upigaji kura wa Oktoba 29.

 

Chanzo: Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: