Kufuatia siku kadhaa za machafuko katika miji mbalimbali nchini Tanzania, maisha yameonekana kurudi kawaida lakini vikosi vya usalama vimeonekana vikishika doria katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.
BBC imeshuhudia maafisa wa polisi na wanajeshi wakiwa katika vituo vya mwendekasi, ofisi ya serikali na maeneo ya biashara kama vituo vya kujaza mafuta wakiwa na silaha pamoja na magari.
Hali hii inafuatia vurugu zilizotokea kuanzia Jumatano ya tarehe 29, siku ambayo Tanzania iliingia kufanya uchaguzi mkuu wa kumchagua rais, wabunge na madiwani.
Kwa mujibu wa mashirika ya haki za binadamu yanaeleza kuwa mamia ya watu wameuwawa katika vurugu hizo, huku serikali ya Tanzania ikikiri kutokea kwa vurugu lakini bado haijatoa idadi kamili ya waliouwawa.
Chanzo; Bbc