Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Shamba la Bangi Hekta 2.5 Lateketezwa Moro

Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro limefanikiwa kuteketeza shamba la bangi lenye ukubwa wa hekta 2.5 katika operesheni ya kudhibiti dawa za kulevya iliyofanyika jana Disemba 27,2025.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro iliyotolewa leo Disemba 28, operesheni hiyo ilifanyika katika eneo la Mnyika, Kijiji cha Chonwe, kata ya Vidunda, Wilaya ya Kipolisi Ruhembe.

“Katika tukio hilo, Festo steven Maneno (30), mkulima na mkazi wa Mnyika alikamatwa katika shamba hilo akifanya shughuli mbalimbali,” taarifa ya Polisi imebainisha.

Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro limesema jitihada za kumsaka mmiliki wa shamba hilo, Peter Christian Ngomawenja zinaendelea ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake. 

 

 

 

Chanzo; Eatv

Kuhusiana na mada hii: