Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Taarifa za Vitisho kwa Dkt. Kitima Hazijapokelewa

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Jumanne Muliro amesema hawajapokea taarifa yoyote kutoka kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Dkt. Charles Kitima juu ya madai ya kutaka kuuliwa.

Akijibu swali la Mwandishi wa AyoTV leo Kamanda Muliro alisema “Ndio nimesikia kutoka kwako, kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda kila Mtu wakiwemo Ma-Father”.

Itakumbukwa hivi karibuni, Padri Kitima alisikika akizungumzia hofu ya maisha yake wakati akimtambulisha Naibu Katibu Mkuu mpya wa Baraza hilo Padri Dkt. Faustine Furaha wa Jimbo Katoliki Moshi ambaye amechukua nafasi ya Padri Chesco Msaga aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Kristo Duniani.

 

Chanzo; Millard Ayo

Kuhusiana na mada hii: