Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Clemence Mwandambo Mikononi Mwapolisi kwa Tuhuma za Kukashifu Dini

Baada ya taarifa kuzaga ndani ya mitandao ya kijamii zikimuulizia mwanamitandao maarufu Clemence Mwandambo Jeshi la Polisi lasafisha anga hilo.

Ambapo taarifa zinasema, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Awali ya "Saint Clemence" ndugu Clemence Kenani Mwandambo, mkazi wa Uzunguni "A". Jijini Mbeya kwa tuhuma za kuchapisha na kusambaza taarifa za uongo pamoja na kukashifu imani za dini zingine.

Mtuhumiwa alikamatwa mnamo Disemba 29, 2025 saa 4:00 asubuhi maeneo ya Uzunguni. Jijini Mbeya akichapisha na kusambaza taarifa za uongo pamoja na kukashifu imani ya dini ya kiislamu na kikristo kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Upelelezi unakamilishwa ili hatua nyingine za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake.

Chanzo: Tanzania Journal

Kuhusiana na mada hii: