Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Kisa Nyama Mjomba Amfanyia Ukatili Mtoto

 Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa tukio la ukatili dhidi ya mtoto wa miaka 10 katika Wilaya ya Urambo, Mkoa wa Tabora, lililofanyika Machi 2, 2026.

Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, picha zilizosambaa mitandaoni zikimuonesha mtoto akifungwa kamba miguu na mikono kisha kuning’inizwa dirishani zinahusiana na tukio hilo. Mtoto huyo alipelekwa hospitalini kwa matibabu baada ya kuokolewa.

Mtuhumiwa wa tukio hilo ametajwa kuwa Joseph Mbalamwezi Fransis, mkazi wa Imalamakoye B, Urambo, ambaye ni mjomba wa mtoto huyo. Inadaiwa alimchukulia hatua hiyo baada ya mtoto kuangusha nyama aliyokuwa anapika.

Polisi mkoani Tabora wamemkamata mtuhumiwa na wanaendelea na hatua za kisheria.

 

 

Chanzo; Itv

Kuhusiana na mada hii: