Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Hitilafu za Kiundeshaji Chanzo Ajali SGR

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limesema ajali ya treni ya SGR iliyotokea katika eneo la Ruvu Mkoani Pwani asubuhi ya leo Oktoba 23, 2025 wakati ikitokea Jijini Dar es salaam kuelekea Dodoma imesababishwa na hitilafu za kiuendeshaji ambazo zilipelekea mabehewa matatu (3) kuacha njia.

Ajali hiyo imetokea leo majira ya saa 2:00 asubuhi na hakuna aliyejeruhiwa licha ya hofu iliyowapata abiria wachache kufuatia ajali hiyo.

Taarifa ya TRC imeeleza kuwa timu ya wataalamu ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Uchukuzi, Mkurugenzi Mkuu TRC na vyombo vya usalama na menejimenti ya TRC wanaendelea na uchunguzi wa kina sambamba na kuhakikisha huduma zinarejea kwa haraka.

 

Chanzo: Eatv

Kuhusiana na mada hii: