Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Niffer Adaiwa Kuhamasisha Fujo

Baada ya Jeshi la Polisi kuthibitisha jioni hii kuwa linamshikilia Mfanyabiashara Jenifer Jovin ( Niffer ), Kamanda wa Polisi Kandaa maalum ya Dar es salaam Jumanne Muliro ametaja tuhuma zinazomkabili Mfanyabiashara huyo mwenye ushawishi mkubwa mitandaoni kuwa ni pamoja na kutuhumiwa kujihusisha kuhamasisha Watu kufanya fujo siku ya kupiga kura.

Kwenye mahojiano na Mwandishi Paschal Mwakyoma wa Ayo Tv Muliro amesema tuhuma nyingine ni tuhuma za kuhamasisha Watu kuchoma Vituo vya mafuta “anatuhumiwa Watu kuwashambulia Maafisa wa Polisi na vitendo vingine vya vurugu kwa njia ya mitandao na njia nyingine mbalimbali ambazo tutatoa ushahidi wake Mahakamani. na kwasababu hizo baada ya kufuatilia amekamatwa na Jeshi la Polisi na anahojiwa”

“Una swali lingine kuhusu Niffer ambaye ulikuwa unamuelezea ? kwako ni Mfanyabiashara, kwa Jeshi la Polisi ni Mtuhumiwa”  amemalizia Kamanda Muliro.

 

Chanzo: Millar Ayo

Kuhusiana na mada hii: