Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Tatizo la Maji Dar es Salaam Serikali Kutoa Majibu

Waziri Mkuu wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, ameiagiza Wizara ya Maji na mamlaka husika kufanya jitihada za dhati kuhakikisha miradi mikubwa ya kimkakati ya Kidunda na Rufiji inakamilika kwa wakati ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro.

Dkt. Nchemba ametoa maagizo hayo alipotembelea na kukagua hali ya uzalishaji wa maji katika Mtambo wa Ruvu Chini, uliopo Bagamoyo mkoani Pwani, ambao ulikuwa umekumbwa na changamoto ya kupungua kwa kiwango cha maji kutokana na ukame uliojitokeza miezi iliyopita.

Aidha, Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Aweso amemuomba Waziri Mkuu upatikanaji wa fedha wa haraka kwa ajili ya kukamilisha mradi wa bwawa la Kidunda ili kumaliza kabisa changamoto ya upungufu wa huduma ya maji inayoweza kujitokeza tena kwa miaka ijayo.

 

 

Chanzo; Itv

Kuhusiana na mada hii: