Ulaya imeendelea kukumbwa na wimbi kali la joto, huku rekodi mpya za viwango vya juu vya halijoto vikiendelea kuvunjwa katika maeneo mbalimbali ya bara hilo mwishoni mwa wiki.
Nchini Ujerumani, hali joto ya awali iliyovunja rekodi ilifikia nyuzi 41.5 za Selsiasi katika eneo la Möckern-Drewitz, lililopo jimbo la mashariki la Saxony-Anhalt, kwa mujibu wa Huduma ya Hali ya Hewa ya Ujerumani.
Shirika la hali ya hewa duniani imeonya kuwa wimbi hilo la joto litakuwa na athari kubwa kwa afya za watu na mifumo ya ikolojia, huku likiongeza hatari ya magonjwa yanayosababishwa na joto kali, moto wa nyika na uharibifu wa mazingira.
Joto kali Ulaya
- Chanzo:
- BBC Swahili