Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Tshisekedi Asema Rwanda Aiheshimu Mikataba ya Amani

Mkutano wa dharura kuhusu mgogoro wa mashariki mwa Kongo, ulioongozwa na Rais wa Uganda Yoweri Museveni, ulimalizika jana Jumapili katika Ikulu ya Entebbe.

Wajumbe kutoka Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo walikubaliana kwamba mataifa ya Maziwa Makuu yanapaswa kuhusishwa kikamilifu katika juhudi za kuutatua mgogoro huo, ambao sasa umeanza kuihusisha Burundi moja kwa moja.

Rais Félix Tshisekedi, aliyehutubia mkutano huo kwa njia ya mtandao, alielezea masikitiko yake kwamba mikataba mbalimbali—ikiwemo ile ya Nairobi, Doha na Washington—haijaheshimiwa na Rwanda pamoja na waasi wa M23.

Amesisitiza kuwa kutotekelezwa kwa makubaliano hayo kunazidi kuchochea mzozo wa mashariki mwa Kongo na kuhatarisha juhudi za kurejesha utulivu katika eneo hilo. 

 

Chazo; Dw

Kuhusiana na mada hii: