Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Trump Avunjwa Moyo na Putin

Rais Donald Trump wa Marekani ameelezea kuvunjwa moyo kwa kutosonga mbele juhudi zake za kumaliza vita vya Ukraine. Kiongozi huyo amesema licha ya kufanya mazungumzo kwa njia ya simu ya kila wakati na hata kukutana na Rais Vladimir Putin wa Urusi, jitihada zake za kumaliza vita hivyo zimeambulia patupu.

“Kila nikizungumza na Vladimir (Putin)  majadiliano huwa mazuri lakini hayatufikishi popote. Nadhan sasa ni wakati sahihi (wa kuweka vikwazo).”

Matamshi yake ameyatoa baada ya serikali yake kutangaza vikwazo vipya vya kiuchumi dhidi ya Urusi vikizilenga kampuni kubwa mbili za mafuta. Trump pia alitangaza mapema wiki kuwa mkutano wake na Putin uliopangwa kufanyika mjini Budapest nchini Hungary umeahirishwa kwa muda usiojulikana.

 

Chanzo: Dw

Kuhusiana na mada hii: