Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Sirikit Malkia wa Thailand Afariki Dunia

Malkia Mstaafu wa Thailand, Sirikit ambaye pia ni mama wa Mfalme wa sasa taifa hilo, Mfalme Vajiralongkorn, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 93.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Kifalme ya Thailand (Thai Royal Household Bureau), Malkia Sirikit amefariki dunia akiwa katika hospitali moja jijini Bangkok siku ya Ijumaa.

Malkia Sirikit, alikuwa akipatiwa matibabu tangu mwaka 2019, kutokana na maradhi yaliyokuwa yakimsumbua ikiwemo maambukizi ya damu.

Kwa zaidi ya miaka 60, Malkia Sirikit alikuwa mke wa Mfalme Bhumibol Adulyadej, ambaye alikuwa mtawala aliyeongoza Thailand kwa muda mrefu zaidi hadi kufariki kwake mwaka 2016.

 

Chanzo: Eatv

Kuhusiana na mada hii: