Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Marekani itazimiliki Meli za Mafuta Ilizozikamata

Rais Donald Trump wa Marekani amesema meli za mafuta ambazo aliamuru zikamatwe nje kidogo mwa pwani ya Venezuela zitabakia kuwa mali ya Marekani.

Akijibu maswali ya waandishi habari mjini Washington, Trump amesema serikali yake itachukua umiliki wa meli hizo na kuashiria kwamba zinaweza kutumika kuhifadhi mafuta.

Tangu Disemba 10, Marekani imezikamata meli mbili za mafuta inazozituhumu kukwepa vikwazo vya Washington kwa biashara ya mafuta ya Venezuela.

Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amezitaja hatua hizo za Marekani kuwa "vitendo vya kijambazi na uharamia wa kimataifa".

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: