Jenerali wa Iran, Kioumars Heydari ameapa kuwa Iran haitaacha vita hivi hadi itakapofikia malengo yake na kutoa mapigo makali dhidi ya Marekani.
“Haijalishi kwetu vita hivi vitadumu kwa siku ngapi,” amesema Heydari, Naibu Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbia Central Headquarters, katika kauli iliyoripotiwa na shirika la habari la nusu rasmi la Iran, Tasnim News Agency.
“Tayari tumewahi kupitia vita vya miaka minane, na tutamaliza vita hivi tu pale tutakapokuwa tumefikia malengo yetu na kumfanya adui ajutie na kukata tamaa kutokana na kitendo chake cha aibu.”
Chanzo; Mwananchi