Watu 169 wakiwemo maafisa wakuu wa Sudani Kusini wameuawa nchini humo katika shambulio lililotekelezwa na Kundi la watu wasiojulikana walioshambulia eneo moja kaskazini mwa nchi hiyo siku ya Jumapili.
Waziri wa Habari Ruweng James Monyluak Mijok amedai kwamba watu hao wametoka katika jimbo jirani la Unity na walikuwa na uhusiano na Jeshi la Ukombozi la Watu wa Sudan katika Upinzani (SPLA-IO).
SPLA-IO imekanusha kuhusika na shambulio hilo, ikishutumu mamlaka ya jimbo la Unity kwa kuingiza siasa kwenye ghasia hizo.
Umoja wa Mataifa umeonya mara kwa mara kuwa nchi hiyo iko katika hatari ya kurejea katika vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe.
Chanzo; Eatv