Jeshi la Wanamaji na Jeshi la Anga la Sri Lanka limetumwa kufanya operesheni ya dharura ya uokoaji baada ya meli ya kijeshi ya Iran kutuma ishara ya hatari na kuanza kuzama karibu na pwani ya kisiwa hicho katika Bahari ya Hindi.
Kwa mujibu wa mamlaka za Sri Lanka, vikosi vyao vilianza haraka operesheni ya utafutaji na uokoaji baada ya kupokea ishara ya dharura kutoka meli hiyo ya Iran iliyokuwa na zaidi ya watu 180 ndani yake. Takribani mabaharia 30 wameokolewa na kupelekwa hospitali katika mji wa Galle kwa matibabu, huku juhudi za kuendelea kuwatafuta wengine zikiendelea baharini.
Chanzo; Global Publishers