Saa chache baada ya mtoto wa Ayatollah Ali Khamenei, Mojtaba Khamenei, kuchaguliwa kuwa kiongozi mpya kurithi mikoba ya baba yake, Israel imetangaza kumuwinda kama ilivyokuwa kwa baba yake.
Mojtaba, 56, amechaguliwa kushika wadhifa huo akitajwa kuwa na ushawishi mkubwa kwenye
vikosi vya ulinzi vya Iran.
Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz amesema kuwa Jeshi la Israel litajaribu kumuua kiongozi huyo na wengine watakaoteuliwa Ali Khamenei.
“Yeyote atakayeteuliwa na utawala wa kigaidi wa Iran kuendelea kuongoza mpango wa kuiangamiza Israel, kuitishia Marekani na ulimwengu huru pamoja na nchi za kanda hii, na kuwaonea wananchi wa Iran, atakuwa shabaha ya moja kwa moja ya kuondolewa,” Katz amesema katika taarifa yake.
Katz ameendelea kusema kuwa Israel itaendelea kushirikiana na Marekani kuangamiza uwezo wa Iran na
“kuunda mazingira yatakayowezesha wananchi wa Iran kuuangusha” utawala wao.
Chanzo; Mwananchi