Rais Emmanuel Macron amesema Ufaransa itaongeza idadi ya vichwa vyake vya nyuklia na kushirikiana na nchi nane kusaidia kuilinda Ulaya huku mshirika muhimu wa NATO, Marekani, ikionyesha kujiondoa.
Macron, ambaye alizungumza kutoka kituo cha manowari za nyuklia cha Ile Longue nchini Ufaransa, alisasisha mafundisho ya nyuklia ya nchi hiyo wakati vita vya Urusi dhidi ya Ukraine vikiendelea kuingia mwaka wa tano na washirika wa NATO wakionyesha wasiwasi kuhusu kuyumba kwa dhamira ya Washington.
"Lazima tuimarishe uwezo wetu wa kuzua hofu kupitia nyuklia mbele ya vitisho vingi, na lazima tuitazame kwa kina ndani ya bara la Ulaya, tukiheshimu kikamilifu uhuru wetu," Macron alisema.
Chanzo; Dw