Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Rais wa Zamani Korea Kaskazini Afariki Dunia

Mtu wa pekee nje ya familia ya Kim kuhudumu kama rais asiye na mamlaka nchini Korea Kaskazini, Kim Yong Nam, amefariki dunia.

Haya ni kulingana na shirika la habari la kitaifa la Korea Kaskazini, KCNA, lililotoa tangazo hilo leo.

Kim Yong Nam ambaye alihudumu katika nafasi hiyo chini ya viongozi wote watatu wa nchi hiyo, amefariki dunia jana akiwa na umri wa miaka 97.

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ametoa heshima zake kwa kiongozi huyo mapema leo.

Nam alihudumu katika wadhfa huo kuanzia mwaka 1998 na akastaafu mwaka 2019 na ndiye aliyekuwa kama sura ya diplomasia ya Korea Kaskazini.

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: