Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Makanisa 10,000 Yafungwa kwa Kukiuka Sheria

Serikali ya Rwanda imefunga zaidi ya makanisa 10,000 baada ya kubainika kushindwa kutimiza masharti ya sheria ya mwaka 2018 inayodhibiti uendeshaji wa maeneo ya ibada nchini humo.

Sheria hiyo iliweka masharti mapya yanayohusu afya na usalama wa waumini pamoja na uwazi wa kifedha, sambamba na hitaji la kila mhubiri kuwa na mafunzo ya theolojia kabla ya kuongoza ibada.

Akizungumza na waandishi wa habari, Rais wa Rwanda, Paul Kagame, amesema haoni mchango wa maana wa baadhi ya makanisa katika kutatua changamoto kubwa zinazoikabili dunia, ikiwemo vita na ukosefu wa ajira.

Rais Kagame amebainisha kuwa badala ya kusaidia jamii, baadhi ya makanisa yanatumika kama njia ya kujinufaisha binafsi kwa viongozi wake, hali iliyochangia Serikali kuchukua hatua za kisheria ili kulinda maslahi ya wananchi na kuhakikisha maeneo ya ibada yanaendeshwa kwa misingi inayokubalika kisheria.

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: