Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Wakenya Washawishiwa Kupigana Upande wa Urusi

 Wizara ya mambo ya nje ya Kenya imesema kuwa baadhi ya Wakenya wamekuwa wakishawishiwa ili kwenda kupigana upande wa Urusi katika vita vyake dhidi ya Ukraine.

Katika taarifa iliyosainiwa na waziri wa mambo ya nje wa Kenya Musalia Mudavadi, imebainisha kwamba Wakenya wengi wameishia kuzuiliwa katika kambi za kijeshi nchini Urusi.

Taarifa hiyo imeongeza kwamba vitendo hivyo vinaendeshwa na mawakala na mafisadi ambao wanadai kufanya kazi na serikali na kuwalaghai Wakenya, wanaosafiri hadi Urusi na bila kujua wanajikuta katika operesheni za kijeshi za nchi hiyo.

Serikali ya Kenya imewataka raia kuwa waangalifu na kutotegemea ahadi za ajira kutoka kwa watu au mashirika yasiyo rasmi, hasa yanayodai kuwa na uhusiano na serikali au mashirika ya kimataifa. 

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: