Christian Eriksen alianguka uwanjani leo (7 Juni 2026) katika mechi ya kirafiki kati ya Denmark na Ukraine, dakika ya 65, baada ya kushika kifua chake ghafla. Eriksen alionekana akishika kifua chake kwa mikono yote miwili kabla ya kuanguka chini. Wachezaji wa Denmark na Ukraine walimzunguka ili kumlinda, madaktari wakaingia mara moja kumpa huduma ya dharura. Kupelekea mchezo kusitishwa na baadaye kufutwa rasmi.
Shirikisho la Soka la Denmark limetangaza kuwa Christian Eriksen yuko mzima na salama, baada ya kuanguka uwanjani
Mchezo kati ya Denmark na Ukraine umefutwa, Eriksen alihisi vibaya na kuanguka uwanjani huku wachezaji wote wakikusanyika kumlinda.
Eriksen yuko fahamu na “anaendelea vizuri kulingana na hali ya sasa,” Shirikisho la Denmark limethibitisha kwa habari njema.
Kwa sasa Eriksen yuko njiani kuelekea hospitali lakini yuko fahamu.