Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Ronaldo Atua Madridi Shambulizi Riyadh

Ndege binafsi ya Cristiano Ronaldo yenye thamani ya £61 milioni iliondoka Saudi Arabia baada ya shambulizi la drone lililolenga ubalozi wa Marekani mjini Riyadh likiwa ni siku ya nne ya mzozo wa kijeshi unaohusisha Iran.

Ronaldo anaishi Riyadh pamoja na mwenzi wake Georgina Rodriguez na watoto wao watano.

Data za flight tracker zinasema ndege hiyo ya aina Bombardier Global Express ilitumia karibu saa saba kufika Madrid, Spain ikiondoka saa 8:00 na kufika karibu saa 1:00 asubuhi.

Mashambulizi yalisababisha ubalozi wa Marekani kujeruhiwa na uharibifu wa mali na vyombo vya habari vya Iran vikidai kuwa jengo la amri na wafanyakazi huko Bahrain pia limeharibiwa.

Ripoti zinaonyesha kuwa raia wa kigeni wanakimbia Mashariki ya Kati kwa wingi huku safari ya Ronaldo ikithibitishwa na data za ndege kama ishara ya tahadhari kutokana na hali tete ya usalama.

 

 

Chanzo; Bongo 5

Kuhusiana na mada hii: