Klabu ya Liverpool inakabiliwa na uwezekano wa kupoteza hadi pauni milioni 120 (Bilioni 412) iwapo haitafuzu kushiriki michuano ya UEFA Champions League msimu ujao, kwa mujibu wa mtaalamu wa masuala ya fedha za soka, Kieran Maguire.
kiasi hicho kinajumuisha mapato ya zawadi kutoka UEFA, haki za matangazo ya televisheni, mapato ya siku ya mechi pamoja na bonasi kutoka kwa wadhamini.
Kukosa kushiriki mashindano hayo ya kifahari barani Ulaya kunaweza pia kuathiri uwezo wa klabu kuvutia wachezaji wakubwa na kuingia mikataba mipya ya kibiashara yenye thamani kubwa.
Champions League imekuwa chanzo muhimu cha mapato kwa vilabu vikubwa Ulaya na kwa Liverpool kufuzu si tu suala la ushindani bali pia ni nguzo ya nguvu za kifedha kwa klabu hiyo.
Chanzo; Bongo 5