Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Madrid Kumuuza Vinicius Jr

Klabu ya Real Madrid imepanga kumuuza mshambuliaji wa Brazil, Vinícius Júnior, mwenye umri wa miaka 25, mwishoni mwa msimu ujao kufuatia mwenendo wake usioridhisha wakati alipotolewa uwanjani katika mechi ya El Clásico dhidi ya Barcelona.

Katika mechi dhidi ya Barcelona ambayo Real Madrid ilishinda kwa mabao 2-1 mwishoni mwa mwezi Oktoba, Vinicius 'alimuwakia' kocha wake, Xabi Alonso baada ya kumtoa wakati mechi ikiendelea, jambo lililowakasirisha viongozi na mashabiki wa timu hiyo walioanza kushinikiza auzwe kutokana na matukio ya kujirudia ya utovu wa nidhamu.

Vinicius Jr alijiunga na Real Madrid mwaka 2018 akitokea klabu ya Flamengo nchini Brazil, ambako alijulikana kwa kasi, mbwembwe na uwezo wake mkubwa wa kumiliki mpira.

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: