Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Rashiford Aikataa Man United

Mshambuliaji Marcus Rashford ameweka wazi kwamba anataka kuondoka kabisa Manchester United na kubaki Barcelona, baada ya msimu huu kumalizika.

Rashford alijiunga na Barcelona kwa mkopo kutoka Manchester United katika usajili wa majira ya kiangazi, na miamba hiyo ya Cataluña ina chaguo la kumsajili moja kwa moja msimu ujao.

Akiwa tayari amefunga mabao matano katika mechi 12, mashambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ameweka wazi mustakabali wake kabla ya pambano kubwa la El Clásico dhidi ya Real Madrid litakalopigwa keshokutwa Jumapili, Oktoba 26.

Alipoulizwa na ESPN kama anataka kubaki Barcelona, Rashford amesema: “Ndiyo, bila shaka. Ninafurahia kuwa katika klabu hii na naamini kwa yeyote anayependa soka aneipenda klabu hii. Barcelona ni moja ya klabu muhimu katika historia ya mchezo huu. Kwa mchezaji, ni heshima kubwa kucheza hapa.”

 

Chanzo: Mwanaspoti

Kuhusiana na mada hii: