Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Gamondi Apewa Mikoba Taifa Stars

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua Kocha wa Singida Black Stars, Miguel Gamondi, raia wa Argentina, kuwa Kaimu Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars).

Uteuzi huo umefanyika baada ya mkataba wa aliyekuwa kocha wa Taifa Stars, Hemed Morocco kusitishwa kwa makubaliano ya pande zote mbili.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF leo, Novemba 4, 2025, mazungumzo rasmi kati ya TFF na uongozi wa Singida Black Stars yamekamilika.

Gamondi ataanza majukumu yake mara moja, akiiongoza Taifa Stars kuelekea kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika nchini Morocco kuanzia Desemba mwaka huu.

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: