Imefahamika kuwa, beki na nahodha wa Liverpool, Virgil Van Dijk, aliitisha mkutano wa wazi wa wachezaji wenzake, ili kuzungumzia masuala mbalimbali ya timu hiyo, ambayo ilipitia changamoto za kukosa matokeo mazuri, kabla ya ushindi dhidi ya Eintracht Frankfurt, Jumatano Oktoba 22, 2025.
Beki huyo raia wa Uholanzi, amefichua kuwa, yeye ndiye aliyeitisha kikao hicho cha wachezaji ambacho kocha Arne Slot hakuhudhuria kufuatia kichapo cha mabao 2-1 kilichotolewa na Manchester United mwishoni mwa wiki iliyopita, ikiwa ni kipigo cha nne mfululizo kwa Liverpool msimu huu.
Van Dijk anaamini mazungumzo hayo yalichangia ushindi mnono wa mabao 5-1 dhidi ya Eintracht Frankfurt iliyokuwa nyumbani nchini Ujerumani, kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Chanzo: Mwanaspoti