Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Yanga Yakimbilia Zanzibar Ligi ya Mabingwa

Yanga imeamua kucheza mechi zake za hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Ofisa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe amesema kuwa uamuzi huo umekuja baada ya tathmini ambayo uongozi wa klabu hiyo umeifanya baada ya kupangwa kwa makundi ya mashindano hayo.

Yanga imepangwa katika kundi B la mashindano hayo ikiwa na timu za Al Ahly (Misri), AS FAR (Morocco) na JS Kabylie (Algeria).

“Ukiangalia hilo kundi ambalo lina timu nne, kundi B ni kundi ambalo kila mmoja ambaye anafahamu mpira, kila mmoja ambaye anafuatilia mpira wa Afrika vizuri na kila mtu ambaye anafuatilia kwa ukaribu ubora wa ngazi ya klabu Afrika, atakiri kwamba kundi hili ni gumu na kwa lugha ya kimpira tunaliita kundi la kifo.

“Sio kundi jepesi na sio kundi lelemama na sisi uongozi wa Young Africans tunakiri kwamba hili ni kundi gumu na ni kundi ambalo halitabiri hadi sasa hivi na yoyote anaweza kuwa na nafasi ya kuelekea kwenye hatua ya robo fainali.

“Na sisi kama klabu tunaanza mipango yetu sasa hivi kuhakikisha tunakuwa timu moja katika mbili ambazo zitafuzu kuelekea hatua ya robo fainali. Tayari ratiba imeshatangazwa kwa maana mechi zitakavyokuwa. Young Africans tutaanzia mchezo wa kwanza nyumbani dhidi ya FAR Rabat, baada ya hapo tutasafiri kwenda Algeria kucheza na JS Kabylie,” amesema Kamwe.

Kamwe amesema kuwa mechi tatu za hatua ya makundi watacheza New Amaan Complex hivyo mashabiki wa soka visiwani Zanzibar wajiandae kuipokea timu hiyo.

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: