Klabu ya Young Africans SC imeendelea kuonyesha ubora wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Singida BS katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa leo katika dimba Airtel Stadium, Singida.
Katika mchezo mwingine, Azam FC imelazimishwa sare ya 0-0 na TZ Prisons, baada ya timu hizo kushindwa kupata bao katika dakika 90 za mchezo huo.
Matokeo hayo yanaifanya Yanga kuendelea kujiimarisha katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
Chanzo; Global Publishers