Diamond kwenye list ya wasanii wenye ushawishi Zaidi barani Afrika
Staa wa Muziki wa Bongo Fleva Diamond Platnumz Ametajwa kwenye List ya Wasanii wenye Ushawishi Mkubwa zaidi Barani Afika Ndani ya Muongo Mmoja uliopita Akiwa nafasi ya Nne.
Kwa mujibu wa tathmini hiyo, nafasi za wasanii hazikupangwa kwa kuangalia umaarufu pekee, bali zilizingatia mchango wao katika kukuza na kuendeleza tasnia ya muziki barani Afrika, uwezo wao wa kuvuka mipaka ya nchi zao, ushawishi wa kazi zao katika mataifa mbalimbali ya Afrika pamoja na mafanikio yao katika soko la kimataifa.