Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Wasiwasi wa Chidi Benzi kuichanganya sanaa yake na siasa

Msanii wa Bongo Fleva Rashid Makwiro almaarufu Chid Benz anasema kwasababu yeye kama msanii ni wa jamii yote hivyo licha ya kutafutwa na vyama mbalimbali vya siasa lakini amekuwa akikataa mialiko hiyo.

Chidi Benz anasema kuwa “Natamani hizo pesa lakini naangalia, watu wananiuliza. Sijawahi kitu chochote cha kuhusiana na Chama.”

“Nimepigiwa na vyama vitatu kwenda kufanya matamasha, sijawahi kukubaliana nao chochote naogopa nionekane nimebagua.” - Chidi Benzi

Chidi Benz amerejea kutoka nyumba ya nafuu ‘Sober House’ siku za hivi karibuni na ameonekana kuimarika kiafya na sasa anajidhatiti kurejea tena kwenye muziki kwa kishindo kama ilvyokua awali alipokua akitamba na vibao kama ngoma itambae na mashallaah.

 

Chanzo: Bbc

Kuhusiana na mada hii: