Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Bonge la Dada Akiri Kutopenda Anachofanya “Unenguaji”

Dansa anayetikisa kupitia wimbo wa Mbosso Khan “Aviola”, Queen Fraison, amefunguka kuhusu kazi yake ya unenguaji ambayo kwa sasa ndiyo inampa zaidi kipato.

Queen Fraison amesema, hapendi kucheza hadharani au kujidhalilisha, lakini hana budi kuendelea nayo kwani ndiyo kazi inayomuweka mjini.

“Sipendi kucheza hadharani au kujidhalilisha, mimi nina familia na nina wazazi kama watu wengine, lakini sina jinsi kwa sababu hii ni kazi inayolipa na siwezi kuiacha, hata familia yangu pia inalijua hilo,” amesema.

Fraison ameeleza kuwa wengi hawajui umaarufu alioupata umetokana na sanaa ya kucheza, na kwa sasa amekuwa akipata mialiko mbalimbali ya maonyesho kupitia kipaji chake hicho.

 

Chanzo: Mwanaspoti

Kuhusiana na mada hii: