Msanii Mulla OBO, ambaye alikuwepo wakati moto ukiteketeza studio za Mwanamuziki Barnaba Classic, amesema hawakufanikiwa kuokoa mali yoyote ndani ya studio hiyo.
Akizungumza na @ayotv_ Mulla OBO ambaye yupo chini ya lebo ya Barnaba, amesimulia namna moto huo ulivyoanza hadi kuiteketeza studio yote.
“Moto ulipoanza nilikuwa na Producer wangu ananirekebishia kitu kwenye simu yangu, nikaona moto ukiwaka kwenye vitambaa vilivyokuwa pembeni, nikamstua ndugu yangu Producer na tulipoona moto umekuwa mkubwa tulitoka nje kupiga kelele kuomba msaada, lakini hatukufanikiwa kuokoa chochote zaidi ya mimi kujitosa kwenda kuchukua simu,” amesema Mulla OBO.