Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando ‘Baba Levo’ amesema kuna baadhi ya Wanawake wanatumika kuwarekodi Viongozi wanapokuwa nao katika mazingira ya faragha.
Akizungumza Bungeni jijini Dodoma, Baba Levo amesema “Kuna Wanawake wanatumwa kwenda kumrekodi Kiongozi hotelini akiwa katika hali ya faragh, inawezekana mtu amefanya makosa yake binafsi, lakini unaenda kwenye simu ya Binti wakati umetoka kuoga unamkuta anakurekodi, utafanyaje, utapeleka simu polisi?”
Kauli hiyo imeibua mjadala bungeni kuhusu maadili, faragha na matumizi ya Teknolojia katika kuwalinda au kuwahatarisha Viongozi na wananchi kwa Ujumla.