Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Bila Email Hautaweza Kutumia Window 11

Windows 11 sasa haitaruhusu tena watumiaji kutumia mfumo huo bila kuwa na akaunti ya barua pepe.

Awali, watumiaji waliweza kuanza kutumia Windows kwa kuunda local account bila kujisajili mtandaoni.

Hata hivyo, Microsoft imetangaza kuondoa kabisa njia ya bypass kwenye hatua ya Out of Box Experience (OOBE). Hii ina maana kwamba kila mtumiaji atalazimika kuingia au kujisajili kwa kutumia akaunti ya barua pepe wakati wa usakinishaji wa mfumo.

Hatua hii inalenga kuimarisha usalama na kurahisisha huduma za mtandaoni, lakini pia inalazimisha watumiaji wote kuwa na akaunti ya Microsoft.

 

Chanzo: Mwananchi Scoop

Kuhusiana na mada hii: