Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Zaidi ya 30,000 Wajisajili Tamasha la Kimataifa la Vijana Urusi

Zaidi ya vijana 30,000 wamewasilisha maombi ya kushiriki Tamasha la Kimataifa la Vijana (World Youth Festival Assembly 2026) litakalofanyika jiji la Yekaterinburg. Uzinduzi wa kampeni ya maombi ulifanyika Februari 5 katika Russia National Centre wakati wa marathon ya “Russia – Family of Families” iliyoandaliwa na Russian Society Znanie. Tukio hilo lilikuwa mwanzo wa kampeni ya kimataifa ya kuwatafuta washiriki wa tamasha hilo la vijana.

Waandaaji wamesesema tamasha hilo litawakutanisha washiriki 10,000, wakiwemo vijana 5,000 kutoka Urusi na 5,000 kutoka nchi nyingine, wanaowakilisha sekta mbalimbali kama vile tasnia za ubunifu, utawala wa umma, sayansi na elimu, michezo, ujasiriamali, vyombo vya habari, teknolojia za kidijitali na sekta ya kijamii.

Mpango huo pia utajumuisha washiriki vijana wenye umri wa miaka 14 hadi 17, ambapo 500 watatoka Urusi na 500 kutoka nchi za nje. Mwaka 2025, World Youth Festival Assembly 2025 ilifanyika katika Nizhny Novgorod na kukusanya takribani washiriki 2,000.

Kwa mujibu wa Grigory Gurov, mkuu wa Rosmolodezh, mwitikio wa vijana duniani umekuwa mkubwa, ambapo zaidi ya maombi 30,000 kutoka nchi 168 yalipokelewa ndani ya mwezi mmoja tangu kufunguliwa kwa usajili, ikiwa ni pamoja na takribani maombi 14,000 kutoka kwa raia wa kigeni.

Ili kuongeza uelewa kuhusu tukio hilo, zaidi ya matukio 450 ya utangazaji yamefanyika nchini Urusi na katika nchi nyingine. Ndani ya Urusi pekee, zaidi ya vijana 62,000 wamepata taarifa kuhusu tamasha hilo kupitia shughuli mbalimbali kama vile maswali na majibu, warsha, mikutano na wanafunzi pamoja na mashindano ya michezo.

Tamasha hilo litafanyika chini ya kaulimbiu “Follow Your Dream. Together with Russia” (Fuata Ndoto Yako, Pamoja na Urusi). Waandaaji wanasema tukio hilo litakuwa jukwaa la mazungumzo ya kimataifa, kubadilishana tamaduni na kuimarisha ushirikiano, huku pia likionyesha miradi na mafanikio mbalimbali ya Urusi.

Tamasha hilo tayari limewasilishwa kwa vijana katika zaidi ya nchi 40, zikiwemo Morocco, Tunisia, India, Kenya, Zambia, Turkey, Argentina na Tanzania. Baadhi ya waombaji kutoka nchi mbalimbali tayari wameeleza matarajio yao kuhusu kushiriki katika tamasha hilo. Sofia Tsvetanova, mtafiti mdogo na mwanafunzi wa shahada ya uzamili katika RUDN University kutoka Bulgaria, alisema anaamini tamasha hilo litasaidia kuimarisha uhusiano kati ya vijana duniani.

Kwa upande wake, Benedetta Armando, mwanafunzi wa uzamili kutoka Italy aliyeshiriki katika mkutano wa vijana wa mwaka 2025 huko Nizhny Novgorod, alisema majukwaa kama hayo hutoa fursa kwa vijana kutoka nchi mbalimbali kubadilishana mawazo kuhusu changamoto za dunia.

Baada ya programu kuu ya tamasha katika Yekaterinburg, washiriki 1,000 kutoka nje ya Urusi watashiriki katika programu maalum ya safari za kikanda. Jumla ya misafara 30 itatembelea maeneo mbalimbali ya Urusi pamoja na Republic of Abkhazia, ambapo vijana wataweza kuona vivutio vikuu, kujifunza kuhusu maendeleo ya teknolojia, pamoja na historia na urithi wa kitamaduni wa nchi hiyo.

Usajili wa tamasha hili unaendelea kupitia tovuti ya wyffest.com.

Kuhusiana na mada hii: